1 “Nimefanya agano na macho yangu
2 Kwa kuwa fungu la mwanadamu ni gani kutoka kwa Mungu juu,
3 Je, si uharibifu kwa watu waovu,
4 Je, yeye hazioni njia zangu
5 “Kama nimeishi katika uongo
6 Mungu na anipime katika mizani za uaminifu,
7 kama hatua zangu zimepotoka kutoka kwenye njia,
8 basi wengine na wale nilichokipanda,
9 “Kama moyo wangu umeshawishiwa na mwanamke,
10 basi mke wangu na asage nafaka ya mwanaume mwingine,
11 Kwa kuwa hilo lingekuwa aibu,
12 Ni moto uwakao kwa Uharibifu;
13 “Kama ningewanyima haki watumishi wangu wanaume au vijakazi wangu,
14 nitafanya nini Mungu atakaponikabili?
15 Je, yeye aliyeniumba tumboni mwa mama yangu,
16 “Ikiwa nimewanyima maskini haja zao,
17 kama nimekula chakula changu mwenyewe,
18 lakini tangu ujana wangu nimemlea yatima kama ambavyo baba angefanya,
19 kama nilimwona yeyote akiteseka kwa kukosa nguo,
20 ambaye wala moyo wake haukunibariki
21 na kama nimeinua mkono wangu dhidi ya yatima,
22 basi mkono wangu na unyofoke toka begani mwangu,
23 Kwa kuwa niliogopa uharibifu kutoka kwa Mungu,
24 “Kama nimeweka tumaini langu kwenye dhahabu,
25 kama nimefurahia wingi wa utajiri wangu,
26 kama nimelitazama jua katika kungʼaa kwake
27 hivyo moyo wangu kushawishiwa kwa siri,
28 basi hiyo pia ingekuwa dhambi ya kuhukumiwa,
29 “Kama nimeshangilia msiba wa adui yangu,
30 lakini sikuruhusu kinywa changu kufanya dhambi
31 kama watu wa nyumbani mwangu kamwe hawakusema,
32 Lakini hakuna mgeni aliyelala njiani,
33 kama nimeifunika dhambi yangu kama wanadamu wengine wafanyavyo,
34 kwa sababu ya kuogopa umati wa watu,
35 (“Laiti kama angekuwepo mtu wa kunisikia!
36 Hakika ningeyavaa begani mwangu,
37 Ningempa hesabu ya kila hatua yangu,
38 “Kama nchi yangu inalia dhidi yangu,
39 kama nimekula mazao yake bila malipo,
40 basi miiba na iote badala ya ngano,