1 “Kwa hili moyo wangu unatetemeka,
2 Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake,
3 Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote
4 Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake;
5 Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu;
6 Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’
7 Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake,
8 Wanyama hujificha;
9 Dhoruba hutoka katika chumba chake,
10 Pumzi ya Mungu hutoa barafu,
11 Huyasheheneza mawingu kwa maji,
12 Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake,
13 Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu,
14 “Ayubu, sikiliza hili;
15 Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu,
16 Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia,
17 Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako
18 je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga,
19 “Tuambieni yatupasayo kumwambia;
20 Je, aambiwe kwamba nataka kuongea?
21 Basi hakuna awezaye kulitazama jua,
22 Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu;
23 Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza;
24 Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni,