Números 1
Biblica® Toleo Wazi Neno: Bibilia Takatifu™ (SWHONEN) vs NTLH
1 Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
1 No segundo ano depois da saída dos israelitas do Egito, no dia primeiro do segundo mês, o Senhor Deus falou com Moisés no deserto do Sinai, na Tenda Sagrada . Ele disse:
2 “Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
2 — Você e Arão devem fazer a contagem do povo de Israel por grupos de famílias e por famílias.
3 Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
3 Façam a lista de todos os homens de vinte anos para cima, isto é, todos os que já têm idade para o serviço militar.
4 Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
4 Vocês chamarão um chefe de grupo de famílias de cada tribo para ajudá-los. São estes os nomes dos homens que vão ajudar vocês: Esses foram os chefes de tribo escolhidos no meio do povo de Israel para representar os seus grupos de famílias.
5 Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia:
5 — ausente —
6 kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
6 — ausente —
7 kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
7 — ausente —
8 kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
8 — ausente —
9 kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
9 — ausente —
10 kutoka wana wa Yosefu:
10 — ausente —
11 kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
11 — ausente —
12 kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
12 — ausente —
13 kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
13 — ausente —
14 kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
14 — ausente —
15 kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
15 — ausente —
16 Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
16 — ausente —
17 Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
17 — ausente —
18 wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
18 — ausente —
19 kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
19 Assim, a contagem no deserto do Sinai foi feita como o Senhor havia ordenado a Moisés. Os homens de vinte anos para cima, que tinham idade para o serviço militar, foram registrados pelo seu nome, cada um no seu grupo de famílias e na sua família. Começaram pela tribo de Rúben, o filho mais velho de Jacó. A soma total das tribos foi a seguinte: Da tribo de Rúben, quarenta e seis mil e quinhentos homens.
20 Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli:
20 — ausente —
21 Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
21 — ausente —
22 Kutoka wazao wa Simeoni:
22 — ausente —
23 Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
23 — ausente —
24 Kutoka wazao wa Gadi:
24 — ausente —
25 Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
25 — ausente —
26 Kutoka wazao wa Yuda:
26 — ausente —
27 Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
27 — ausente —
28 Kutoka wazao wa Isakari:
28 — ausente —
29 Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
29 — ausente —
30 Kutoka wazao wa Zabuloni:
30 — ausente —
31 Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
31 — ausente —
32 Kutoka wana wa Yosefu:
32 — ausente —
33 Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
33 — ausente —
34 Kutoka wazao wa Manase:
34 — ausente —
35 Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
35 — ausente —
36 Kutoka wazao wa Benyamini:
36 — ausente —
37 Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
37 — ausente —
38 Kutoka wazao wa Dani:
38 — ausente —
39 Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
39 — ausente —
40 Kutoka wazao wa Asheri:
40 — ausente —
41 Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
41 — ausente —
42 Kutoka wazao wa Naftali:
42 — ausente —
43 Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
43 — ausente —
44 Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
44 — ausente —
45 Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
45 — ausente —
46 Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
46 — ausente —
47 Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
47 Mas os levitas não foram registrados com as outras tribos ,
48 Bwana alikuwa amemwambia Mose:
48 pois o Senhor tinha dito a Moisés o seguinte:
49 “Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
49 — Quando você fizer a contagem dos homens com idade para o serviço militar, deixe de fora os homens da tribo de Levi.
50 Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
50 Mas ponha os levitas para cuidarem da Tenda Sagrada e de todos os seus móveis e objetos. Eles carregarão a Tenda e todo o seu equipamento, farão ali o serviço religioso e acamparão ao redor dela.
51 Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
51 Quando a Tenda tiver de ser transportada, os levitas a desarmarão e, quando for preciso acampar de novo, eles a armarão outra vez. Quem não for levita e chegar perto da Tenda deverá ser morto.
52 Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
52 Os outros israelitas ficarão cada um no seu próprio acampamento, perto da sua própria bandeira, de acordo com o seu grupo.
53 Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
53 Mas os levitas acamparão ao redor da Tenda para guardá-la a fim de que ninguém chegue perto, e assim eu não fique irado com o povo de Israel.
54 Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.
54 E o povo fez tudo como o Senhor havia ordenado a Moisés.
Atalhos do teclado
- Capítulo anterior←
- Próximo capítulo→
- Versículo anteriork
- Próximo versículoj
- Limpar seleçãoEsc
- Esta ajuda?
Estude este capítulo no WhatsApp
Peça à IA da Bíblia Fala para explicar Números 1, comparar traduções ou montar um estudo — tudo direto pelo WhatsApp.