Lucas 20

Swahili NT (SWA) vs NTLH

Sair da comparação
NTLH Nova Tradução na Linguagem de Hoje 2000
1 Siku moja, Yesu alipokuwa akiwafundisha watu Hekaluni na kuwahubiria juu ya Habari Njema, makuhani wakuu na walimu wa Sheria pamoja na wazee walifika,
1 Certo dia, Jesus estava no pátio do Templo ensinando o povo e anunciando o evangelho . Então chegaram ali alguns chefes dos sacerdotes e alguns mestres da Lei, junto com alguns líderes do povo,
2 wakasema, "Tuambie! Unafanya mambo haya kwa mamlaka gani?"
2 e perguntaram: — Diga para nós: com que autoridade você faz essas coisas? Quem lhe deu essa autoridade?
3 Yesu akawaambia, "Na mimi nitawaulizeni swali:
3 Jesus respondeu:
4 mamlaka ya Yohane ya kubatiza yalitoka kwa Mungu au kwa watu?"
4 Quem deu autoridade a João para batizar? Foi Deus ou foram pessoas?
5 Lakini wao wakajadiliana hivi: "Tukisema yalitoka mbinguni, yeye atatuuliza: `Mbona hamkumsadiki?`
5 Aí eles começaram a dizer uns aos outros: — O que é que vamos dizer? Se dissermos que foi Deus, ele vai perguntar: “Então por que vocês não creram em João?”
6 Na tukisema yalitoka kwa binadamu, watu wote hapa watatupiga mawe, maana wote wanaamini kwamba Yohane alikuwa nabii."
6 Mas, se dissermos que foram pessoas, esta multidão vai nos apedrejar, pois eles acham que João era profeta .
7 Basi, wakamwambia, "Hatujui mamlaka hayo yalitoka wapi."
7 Por isso responderam: — Nós não sabemos quem deu autoridade a João para batizar.
8 Yesu akawaambia, "Hata mimi sitawaambia ninafanya mambo haya kwa mamlaka gani."
8 Jesus disse:
9 Yesu akaendelea kuwaambia watu mfano huu: "Mtu mmoja alilima shamba la mizabibu, akalikodisha kwa wakulima; kisha akasafiri hadi nchi ya mbali, akakaa huko kwa muda mrefu.
9 Depois Jesus contou esta parábola para o povo:
10 Wakati wa mavuno, mtu huyo alimtuma mtumishi wake kwa wale wakulima, akachukue sehemu ya matunda ya shamba la mizabibu. Lakini wale wakulima wakampiga mtumishi huyo wakamrudisha mikono mitupu.
10 Quando chegou o tempo da colheita, ele mandou um empregado para receber a sua parte. Mas os lavradores bateram nele e o mandaram de volta sem nada.
11 Yule bwana akamtuma tena mtumishi mwingine; lakini wao wakampiga huyo vilevile na kumtendea vibaya, wakamrudisha mikono mitupu.
11 O dono mandou outro empregado, mas eles também bateram nele, depois o trataram de modo vergonhoso e o mandaram de volta sem nada.
12 Akamtuma tena wa tatu; huyu naye, baada ya kumwumiza, wakamfukuza.
12 Então ele enviou um terceiro empregado, mas os lavradores também bateram nele e o expulsaram.
13 Yule mwenye shamba akafikiri: `Nitafanya nini? Nitamtuma mwanangu mpenzi; labda watamjali yeye.`
13 Aí o dono da plantação pensou: “O que vou fazer? Já sei: vou mandar o meu filho querido. Tenho certeza de que vão respeitá-lo.”
14 Wale wakulima walipomwona tu, wakasemezana: `Huyu ndiye mrithi. Basi, tumwue ili urithi wake uwe wetu.`
14 — Mas, quando os lavradores viram o filho, disseram: “Este é o filho do dono; ele vai herdar a plantação. Vamos matá-lo, e a plantação será nossa.”
15 Basi, wakamtoa nje ya lile shamba la mizabibu, wakamwua." Yesu akauliza, "Yule mwenye shamba atawafanya nini hao wakulima?
15 — Então eles jogaram o filho para fora da plantação e o mataram. Aí Jesus perguntou:
16 Atakuja kuwaangamiza wakulima hao, na atawapa wakulima wengine hilo shamba la mizabibu." Watu waliposikia maneno hayo, walisema: "Hasha! Yasitukie hata kidogo!"
16 Ele virá, matará aqueles homens e dará a plantação a outros lavradores. Então as pessoas que estavam ouvindo disseram: — Que Deus não permita que isso aconteça!
17 Lakini Yesu akawatazama, akawaambia, "Maandiko haya Matakatifu yana maana gani basi? `Jiwe walilokataa waashi, sasa limekuwa jiwe kuu la msingi!`
17 Mas Jesus olhou bem para eles e disse:
18 Mtu yeyote akianguka juu ya jiwe hilo, atavunjika vipandevipande; na likimwangukia mtu yeyote, litamsaga kabisa."
18 Quem cair em cima dessa pedra ficará em pedaços. E, se a pedra cair sobre alguém, essa pessoa vai virar pó.
19 Walimu wa Sheria na makuhani wakuu walifahamu kwamba mfano huo ulikuwa unawahusu, na hivyo walitaka kumkamata palepale, ila tu waliogopa watu.
19 Os mestres da Lei e os chefes dos sacerdotes sabiam que era contra eles que Jesus havia contado essa parábola e queriam prendê-lo ali mesmo, porém tinham medo do povo.
20 Basi, wakawa wanatafuta wakati wa kufaa. Wakawahonga watu fulani wajisingizie kuwa wema, wakawatuma wamnase Yesu kwa maswali, na hivyo waweze kumtia nguvuni na kumpeleka kwa wakuu wa serikali.
20 Então começaram a vigiar Jesus. Pagaram alguns homens para fazerem perguntas a ele. Eles deviam fingir que eram sinceros e procurar conseguir alguma prova contra Jesus. Assim os mestres da Lei e os chefes dos sacerdotes teriam uma desculpa para o prender e entregar nas mãos do Governador romano.
21 Hao wapelelezi wakamwambia, "Mwalimu, tunajua kwamba unasema na kufundisha mambo ya kweli; tunajua kwamba wewe huna ubaguzi; wewe wafundisha ukweli juu ya njia ya Mungu.
21 Esses homens perguntaram: — Mestre, sabemos que aquilo que o senhor diz e ensina é certo. Sabemos também que o senhor não julga pela aparência e ensina a verdade sobre a maneira de viver que Deus exige.
22 Basi, twambie kama ni halali, au la, kulipa kodi kwa Kaisari!"
22 Diga: é ou não é contra a nossa Lei pagar impostos ao Imperador romano?
23 Yesu alitambua mtego wao, akawaambia,
23 Mas Jesus percebeu a má intenção deles e disse:
24 "Nionyesheni sarafu. Je, sura na chapa ni vya nani?"
24 — Tragam aqui uma moeda. De quem são o nome e a cara que estão gravados nela? — São do Imperador! — responderam eles.
25 Nao wakamjibu, "Ni vya Kaisari." Yesu akawaambia, "Basi, mpeni Kaisari vilivyo vyake Kaisari, na Mungu vilivyo vyake Mungu."
25 Então Jesus disse:
26 Hawakufaulu kumnasa kwa neno lolote pale mbele ya watu na hivyo wakakaa kimya wakilistaajabia jibu lake.
26 Eles não puderam conseguir nenhuma prova contra Jesus diante do povo. Por isso ficaram calados, admirados com a resposta dele.
27 Kisha Masadukayo, ambao husema kwamba wafu hawafufuki, wakamjia Yesu, wakasema:
27 Alguns saduceus , os quais afirmam que ninguém ressuscita, chegaram perto de Jesus
28 "Mwalimu, Mose alituandikia kwamba kama ndugu ya mtu fulani akifa na kumwacha mjane wake bila watoto, ni lazima ndugu yake amchukue huyo mama mjane, amzalie watoto ndugu yake marehemu.
28 e disseram: — Mestre, Moisés escreveu para nós a seguinte
29 Sasa, wakati mmoja kulikuwa na ndugu saba. Yule wa kwanza alioa na baadaye akafa bila kuacha mtoto.
29 Acontece que havia sete irmãos. O mais velho casou e morreu sem deixar filhos.
30 Yule ndugu wa pili akamwoa yule mjane, naye pia, akafa;
30 Então o segundo casou com a viúva,
31 na ndugu wa tatu vilevile. Mambo yakawa yaleyale kwa wote saba--wote walikufa bila kuacha watoto.
31 e depois, o terceiro. E assim a mesma coisa aconteceu com os sete irmãos, isto é, todos morreram sem deixar filhos.
32 Mwishowe akafa pia yule mwanamke.
32 Depois a mulher também morreu.
33 Je, siku wafu watakapofufuliwa, mwanamke huyo atakuwa mke wa nani? Alikuwa ameolewa na wote saba."
33 Portanto, no dia da ressurreição, de qual dos sete a mulher vai ser esposa? Pois todos eles casaram com ela!
34 Yesu akawaambia, "Watu wa nyakati hizi huoa na kuolewa;
34 Jesus respondeu:
35 lakini wale ambao Mungu atawawezesha kushiriki ule wakati wa ufufuo, hawataoa wala kuolewa.
35 Mas as pessoas que merecem alcançar a ressurreição e a vida futura não vão casar lá,
36 Ama hakika, hawawezi kufa tena, kwa sababu watakuwa kama malaika, na ni watoto wa Mungu kwa vile wamefufuliwa katika wafu.
36 pois serão como os anjos e não poderão morrer. Serão filhos de Deus porque ressuscitaram.
37 Lakini, kwamba kuna kufufuka kutoka wafu, hata Mose alithibitisha jambo hilo katika Maandiko Matakatifu. Katika sehemu ya Maandiko Matakatifu juu ya kile kichaka kilichokuwa kinawaka moto, anamtaja Bwana kama Mungu wa Abrahamu, Isaka na Yakobo.
37 E Moisés mostra claramente que os mortos serão ressuscitados. Quando fala do espinheiro que estava em fogo, ele escreve que o Senhor é “o Deus de Abraão, o Deus de Isaque e o Deus de Jacó.”
38 Basi, yeye si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa wale walio hai; maana wale aliowaita kwake, wanaishi naye."
38 Isso mostra que Deus é Deus dos vivos e não dos mortos, pois para ele todos estão vivos.
39 Baadhi ya wale walimu wa Sheria wakasema, "Mwalimu, umejibu vema kabisa."
39 Aí alguns mestres da Lei disseram: — Boa resposta, Mestre!
40 Walisema hivyo kwa sababu hawakuthubutu kumwuliza tena maswali mengine.
40 E não tinham coragem de lhe fazer mais perguntas.
41 Yesu akawauliza, "Yasemekanaje kwamba Kristo ni mwana wa Daudi?
41 Em seguida Jesus perguntou a eles:
42 Maana Daudi mwenyewe anasema katika Zaburi: `Bwana alimwambia Bwana wangu: Keti upande wangu wa kulia
42 Pois o próprio Davi diz assim no livro de Salmos:
43 mpaka niwafanye adui zako kama kiti cha kuwekea miguu yako.`
43 até que eu ponha os seus inimigos
44 Ikiwa Daudi anamwita yeye, `Bwana,` basi atakuwaje mwanawe?"
44 Se Davi chama o Messias de Senhor, como é que o Messias pode ser descendente de Davi?
45 Yesu aliwaambia wanafunzi wake mbele ya watu wote,
45 O povo todo estava escutando, e Jesus disse aos discípulos:
46 "Jihadharini na walimu wa Sheria ambao hupenda kupitapita wamevalia kanzu. Hupenda kusalimiwa na watu kwa heshima masokoni, huketi mahali pa heshima katika masunagogi na kuchukua nafasi za heshima katika karamu.
46 — Cuidado com os
47 Huwadhulumu wajane huku wakisingizia kuwa wema kwa kusali sala ndefu. Hao watapata hukumu kali zaidi!"
47 Exploram as viúvas e roubam os seus bens; e, para disfarçar, fazem orações compridas. Portanto, o castigo que eles vão sofrer será pior ainda!

Ler em outra tradução

Comparar com outra

Estude este capítulo no WhatsApp

Peça à IA da Bíblia Fala para explicar Lucas 20, comparar traduções ou montar um estudo — tudo direto pelo WhatsApp.